Ezekiel 21:28-32

28 a“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao.

“ ‘Upanga, upanga,
umefutwa kwa ajili ya kuua,
umesuguliwa ili kuangamiza
na unametameta kama umeme wa radi!
29 bWakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako,
wanapobashiri uongo kwa ajili yako,
wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu,
wale walio waovu,
wale ambao siku yao imewadia,
wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 cUrudishe upanga kwenye ala yake!
Katika mahali ulipoumbiwa,
katika nchi ya baba zako,
huko nitakuhukumu.
31 dNitamwaga ghadhabu yangu juu yako
na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako;
nitakutia mikononi mwa watu wakatili,
watu stadi katika kuangamiza.
32 eMtakuwa kuni za kuwashia moto,
damu yenu itamwagwa katika nchi yenu,
wala hamtakumbukwa tena;
kwa maana Mimi Bwana nimesema.’ ”
Copyright information for SwhNEN